Monday 27 February 2017

Tuzo za Oscars zilivyozua Mgogoro

Tuzo za Oscars zimezua mgogoro baada ya mchanganyiko wa matokeo uwanjani.
Awali filamu ya kimuziki ya LALA Land ilitangazwa kuwa mshindi wa tuzo hizo.
Lakini cha kushangaza ni kwamba baada ya waigizaji kupanda jukwaani na kusherekea ushindi ghafla mtangazaji alikuja na kutangaza upya.
Mtangazaji aliitangaza filamu ya Moonlight kuwa mshindi wa tuzo hizo.
Filamu ya Moonlight ni filamu inayosimulia hadithi ya mvulana mweusi anayeegemea mapenzi ya jinsia moja.
Hii ilileta purukushani katika hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment