Tuesday 21 February 2017

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe asherehekea kutimiza miaka 93

Rais Robert Mugabe be amekuwa mamlakani tangu nchi hiyo ipate uhuru mwaka 1980
Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, kiongozi wa taifa mwenye umri wa juu zaidi duniani kwa sasa, ametimiza miaka 93.
Kiongozi huyo anatarajiwa kujumuika kwa sherehe ya faradha na jamaa, wafanyakazi wake wa karibu na baadhi ya maafisa wakuu serikali.
Sherehe kubwa rasmi, inayotarajiwa kugharimu zaidi ya dola milioni moja za Kimarekani, itaandaliwa siku ya Jumamosi.
Rais Mugabe aliongoza Zimbabwe kupata uhuru wake mwaka 1980 na ametangaza kwamba anapanga kuwania katika uchaguzi mkuu mwaka ujao, ambapo atakuwa na umri wa miaka 94.
Mugabe alizaliwa 21 Februari, 1924.
Alifungwa jela 1964-1974 kwa kutoa "hotuba ya kuhujumu serikali"

Baada ya kuachiliwa, alisaidia kuongoza vita dhidi ya serikali ya Rhodesia
Vita vilipomalizika, Mugabe alishinda uchaguzi 1980 na akawa waziri mkuu wa Zimbabwe na akaongoza taifa hilo kama waziri mkuu hadi mwaka 1987.

No comments:

Post a Comment