Tuesday 28 February 2017

Mmiliki wa Samsung afikishwa mahakamani kwa kutoa hongo



Mrithi wa kampuni tajiri zaidi nchini Korea Kusini, Samsung, atafikishwa mahakamani kwa madai ya kutoa hongo na ubadhirifu wa pesa, katika sakata kubwa inayoendelea kutokota, ambayo pia imesababisha kutimuliwa kwa rais, Park Guen-hye.
Mwendesha mashtaka maalum amesema kwamba, Lee Jay-yong, pamoja na wakuu wengine wanne wa Samsung watashtakiwa.

Bwana Lee, aliyekamatwa mapema mwezi huu, anashtakiwa kwa madai ya kutoa hongo ya takriban dola milioni 40, kwa mshirika wa karibu wa rais wa zamani, ili kupata usaidizi wa kisiasa.

No comments:

Post a Comment