Friday 24 February 2017

Shule za sekondari hapa nchini zinakabiliwa na changamoto sugu ya kuwepo kwa upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi

Waziri wa  elimu sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako kushoto akiwa na na Mbunge wa Jimbo la Rufiji wa  kulia Mohamed Mchengerwa akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Utete wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kujionea chanagamoto mbazi mbali zinazoikabili sekta ya elimu.
2
Waziri wa elimu Sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako kulia akiwa na baadhi ya viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Rufiji mara baada ya kufanya ziara yake  ya kikazi ya kutembelea shule mbali mbali zilizopo Wilayani Rufiji.
3
Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa aliyesimama akizungumza na walimu wa shule ya sekondari ya Ikwiriri pamoja na walimu wa shule za msingi hawapo pichani,kushoto kwake ni Waziri wa Elimu wa sayansi na Tekonolojia katika ziara hiyo.
4
Baadhi ya viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Rufiji wakiwa katika shule ya sekondari ya Ikwiriri  wakiteta jambo na Wazairi wa  elimu sayansi ya na Tekonolojia Professa Joyce Ndalichako aliyefanya ziara yake ya kutembelea shule mbali mbali Wilaya hiyo.
 NA VICTOR MASANGU, RUFIJI
Shule za sekondari hapa nchini bado zinakabiliwa  na changamoto sugu ya kuwepo kwa  upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi pamoja na kutokuwa na  vifaa vya  maabara kunachangia kwa kiasi kikubwa kushuka na kuzolota  kwa kiwango cha ufaulu kwa  wanafunzi  kutokana na kufanya vibaya katika mitihani yao ya kumaliza  kidato cha nne na sita.
Katika kuliona  hilo Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako alisema  kwamba serikali ya awamu ya tano kwa sasa imeshaanza kufanya mchakato kwa ajili ya kuweza kuanza kusambaza vifaa vya maabara katika shule zipatazo 1625 sambamba na  kuwaajiri walimu wa masomo ya sayansi wapatao 4200 ambao wataweza kuleta mabadiliko chanya katika kuongeza kasi ya ufundushashi.
 Waziri Ndalichoko aliyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi  katika Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani  ambapo aliweza  kutembelea  katika shule tatu za sekondari ikiwemo shule ya Utete,Muhoro pamoja nna Ikwiriri  kwa lengo la kuweza kujionea chagamoto zinazowakabili wanafunzi pamoja na walimu ili kuweza kuzitatutia ufumbuzi wa kudumu.
“Ni kweli changamoto hii ipo ya uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi pamoja na  vifaa vya maabara lakini nipende kuwaahidi kuwa serikali ya awamu ya tano katika kuboresha sekta ya elimu kwa sasa  ipo katika mchakato wa kuana utekeleaji wa kusambaa vifaa vya maabara katika shule 1625 pamoja na kuajri walimu wengine hivyo kwa Wilaya ya Rufiji msiwe na shaka kabisa katika hili,”alisema Ndalichako.
Aidha Prosefa Ndalichako alisema kuwa mchakato huo amabao unatarajiwa kuanza rasmi mwezi wa tatu mwaka huu pia utazigusa na baadhi ya shule za sekondari zilizzopo katika halamashauri ya Wilaya ya Rufiji ili kuweza  kuondokana kabisa na hali hiyo na kuweza kuwapa fursa wanafunzi waweze kufanya vizuri katika mitihani yao bila ya kuwa na vikwazo vyovyote vile.
Aidha Waziri huyo katika hatua nyingine alipiga marufuku kwa wanafunzi wenye tabia ya kuamua  kwenda kukesha katika ngoma  za usiku au kwenda disco na badala yake sasa  amewataka wahakikishe kwamba  wanajikita zaidi katika kuongeza juhudi na mahalifa katika  masomo yao ili kuweza kuongeza kiwango cha ufaulu.


Baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari Utete akiwemo Salum  Salum pamoja na Sarafina Muhina  walisema kwamba kwa sasa wanajikuta wanasoma katika mazingira magumu kutokana na kutokuwa na walimu wa sayansi pamoja na vifaa vya maabara  hivyo kuwasababishia kufanya vibaya katika masomo yao tofauti na matarajio yao.
Pia waliiomba serikali kuweza kuharakisha zoezi hilo la kuwaajiri walimu pamoaj na kugawa vifaa kwa ajili ya maabara ili kuweza kuwafanya kuongeza juhudi katika masomo yao  na kulet mabadiliko ya kuongeza kiwango cha ufaulu katika siku za usoni.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa amebainisha kuwa  sekta ya elimu bado ni tatizo kubwa katika shule za msingi na sekondari hivyo amemwomba Waziri kulivalia njuga suala hilo kwa kuboresha miundombinu ya madarasa, vyoo, pamoja na kuongeza idadi  walimu  ili kuweza kuwapa fursa wanafunzi wawze  kujisomea katika mazingira ambayo ni rafiki kwao.
Pia Mchengerwa alisema kwamba katika jimbo lake shule nyingi za sekondari zinakabiliwa hivyo ataendelea kushirikiana na serikali iliyopo madarakani katika kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingira mazuri kwa lengo la kuweza kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi hao.
 KUSHUKA  kwa kiwango cha elimu hapa nchini  kwa wanafunzi wa shule za sekondari wanaosoma hususan masomo ya sayansi  kunatokana  na kutokuwa na vifaa vya maabara kwa ajili ya kufundishia kwa njia ya vitendo pamoja na uhaba wa walimu.

No comments:

Post a Comment