Sunday 24 January 2016

kam1Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Y. Ndugai (MB) akiongoza kikaoo cha Kamati ya Uongozi ya Bunge-Ofisi za Bunge Mjini Dodoma leo tarehe 24 Januari 2016. Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ni Wenyeviti wote wa Kamati za Kudumu za Bunge.
kam2Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson (MB) akiwasalimia wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge kabla ya kuanza kwa kikaoo.
kam3Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mheshimiwa George Masaju akimsalimia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe (MB) kabla ya kuanza kwa kikaoo cha Kamati ya Uongozi. Kushoto ni Mwwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji Dkt Mary Nagu (MB)
kam5Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mheshimiwa Jenista Mhagama (MB) (aliyesimama katikati) akizungumza na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe (MB) (kushoto) pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mheshimiwa George Masaju (kulia).
kam6Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mheshimiwa George Masaju (kulia) akizungumza na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe (MB) (kushoto) kabla ya kuanza kwa kikaoo cha Kamati ya Uongozi.
kam7Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge ambao ni Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge wakisubiri kuanza kwa kikaoo cha kwanza cha Kamati hiyo.

Mashindano ya Michezo ya Wanafunzi wa Vyuo vikuu yafunguliwa Rasmi jijini Dar es Salaam.

leo1
Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Leonard Tadeo akikabidhi Jezi kwa moja ya timu zinazoshiriki katika mashindano ya michezo yanayohusisha wanafunzi  wa vyuo vikuu  leo jijini Dar es Salaam.Wa kwanza kulia kwake ni mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Dar es Salaam Bw.Imani Matabula.
leo2
Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Leonard Tadeo akikagua timu ya chuo kikuu cha Dar es salaam wanaokaa  Chuoni wakati wa ufunguzi wa mashindano ya michezo ya  vyuo vikuu yanayofanyika katika viwanja vya michezo vya chuo kikuu cha Dar es Salaam.
leo3
Mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Dar es Salaam Bw.Imani Matabula(aliyesimama) akimkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Michezo kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Leonard Tadeo(kushoto) wakati wa ufunguzi  wa mashindano ya michezo ya  vyuo vikuu yanayofanyika katika viwanja vya michezo vya chuo kikuu cha Dar es Salaam.

jal1
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Wabunhe kwenye jengo la utawala la Bunge mjini Dodoma Januari 24, 2016. Kutoka kushoto  ni  Dkt. Raphael Chegeni wa Busega, Adadi Rajabu wa Mhuheza  na Jason Rweikiza wa Bukoba Vijijini. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
jal3
 Waziri Mkuu, Kassim Majlaliwa akizungumza na wenyeviti wa Kamati za Bunge Ofisini kwake mjini Dodoma Januari 24, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
jal4 jal5
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Mbunge wa Busega, Dkt.Raphael Chegeni kwenye jengo la utawala la Bunge mjini Dodoma Januari 24, 2016.

No comments:

Post a Comment