Saturday 30 January 2016


BONDIA mzaliwa wa Tanzania Omari Kimweri ambaye ni bingwa wa uzito wa flyweight nchini Deer Park, Victoria, Australia anatarajia kucheza mpambano wake mwingine  feb 26 akizipiga na  Michael Camellion kutoka Philippines  mpambano wa raundi kumi wa ubingwa wa WBA Pan African light flyweight title .
The Melbourne Pavilion, Flemington, Victoria, Australia
 
Kimweri Mpaka sasa amepanda ulingoni mara 17 tangia aanze kucheza ngumi za kulipwa mwaka 2007 akiwa Ameshinda Michezo 14 na kupoteza michezo 3
 
Bondia huyo Mtanzania anayefanya shughuli zake Australia  amewaomba watanzania kumuombea Dua kwa ajili ya mchezo wake  huo ili afanye vizuri na kushinda Mchezo huo  ambapo baada ya hapo atakuwa na Uwezo wa kupigania Ubingwa wa Dunia wa WBA.
 Kwa kuwa Maandalizi anayoyafanya kwa sasa ni Mazuri na sapoti anayoipata ni nzuri sana 
 Akishinda Mchezo huo itabadilisha maisha ya mchezaji huyo  wa masumbwi na kuwa na kipato kikubwa Wakati akipigania mikanda mikubwa inayotambulika Duniani akianzia na mkanda wa WBA ambao Ameahidiwa kucheza Baada ya kushinda mechi yake hii ya Feb. 26
 
Kimweri alitoa shukrani kwa wadau wanaomsapoti kwa makocha wa Tanzania aliokwisha fanya Nao kazi ambapo mpaka sasa anawakumbuka kwa mchango wao mkubwa kwake katika mchezo Wa Masumbwi, makocha hao ni Baba yake mzazi Idd Kimweri, kaka yake Riadha Kimweri, Habibu Kinyogoli , Rajabu Mhamila ‘Super D’ 
 
Kocha wa Tanzania Prison Remmy Ngabo,Kameda Antony pamoja na Mabondia wa mkoa wa Tanga na Antony Edoa pamoja na kaka zake wote katika mchezo wa masumbwi Twalib Kimweri Mzonge Hassan, Ibrahimu Mashi, na mama zake wote kutoka mkoa wa Tanga 
 
Ambao wamekuwa chachu kwake katika mchezo wa ngumi mpaka amefikia hatua ya kuwa hapo Alipofikia na hata kama anaishi nje ya Tanzania amesema hawezi  kusahau asili yake kwa kuwa kitovu Tanzania ndipo kitovu chake kilipozikiwa.

No comments:

Post a Comment