
Katika taarifa yake iliotolewa baada ya mkutano wa dharura ,kundi hilo limemshtumu mpatanishi wa Umoja wa Afrika Edem Kodjo ambaye linadai anataka kuhakikisha kuwa rais wa sasa Joseph Kabila anawania muhula wa tatu,swala linalokiuka katiba ya taifa hilo.
Kundi hilo sasa limeitisha mgomo siku ya Jumanne,siku ambayo bwana Kodjo,waziri mkuu wa zamani nchini Togo alitaka mazungumzo hayo kufanyika baada ya serikali kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa.

No comments:
Post a Comment