
Basi lilowabeba wachezaji wa Iceland likipita mitaani
Wachezaji walipita katikati ya mji wakiwa ndani ya basi kubwa la wazi wakisindikizwa na ngoma hadi katika mlima wa Arnarholl ambapo mashabiki waliwasalimia kwa shangwa na makofi .
Iceland ambayo imeshiriki kwa mara ya kwanza mashindano makubwa ya Kombe la mataifa barani Ulaya ilifikia ukingoni mwa mashindano mwaka huu baada ya kupata kichapo kutoka kwa Ufaransa kwa magoli 5 - 2.
Hata hivyo kabla ya kuondolewa ilionyesha maajabu pale ilipoiondoa England kwenye hatua ya kumi na sita bora.
No comments:
Post a Comment