Sunday 31 July 2016

IGP Mangu akagua miundombinu ya kipolisi mkoani Shinyanga

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga jana, kulia ni kamanda wa Polisi mkoani humo, Muliro J. Muliro.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifuatilia jambo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Mhe. Fadhil Nkhulu (aliyesimama) anayefuata ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab R. Telack, pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifafanua jambo wakati alipomtembelea ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, Mhe. Simon S. Berege (katikati), akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi, kulia ni kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Muliro J. Muliro.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akiangalia kwa umakini ramani ya mipango miji inayoonesha mahala itakapokuwepo Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, katikati (aliyevaa tai) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Msalala Mhe. Simon S. Berege, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika mkoa wa Shinyanga.

No comments:

Post a Comment