Thursday 28 July 2016

Dayna Nyange.amesema anashindwa kufanya kazi na wasanii wa kike kwa sasa idea nyingi ninazokuwa nazo zinahitaji wasanii wa kiume

 
Wasanii wengi wa kike kwenye muziki hapa Bongo wamekuwa wagumu katika kushirikishana kwenye nyimbo zao, mmoja kati ya wasanii hao ni Dayna Nyange.
Akiongea na  Fofammedia  Dayna amesema kuwa kwa sasa ideas nyingi anazokuwa nazo zinahitaji sana wasanii wa kiume pekee.


“Siwezi kusema kuwa nawatenga wasanii wenzangu wa kike kufanya nao kazi, kila kitu kina wakati wake. Nitafanya nao kazi pale nitakapoona inahitajika nifanye nao kazi. Nashindwa kufanya nao kwa sasa kwa sababu idea nyingi ninazokuwa nazo zinahitaji wasanii wa kiume pekee,” amesema Dayna.

“Lakini nashukuru angalau nilishawahi kufanya kazi na Misoji Nkwabi aliyekuwa mshindi wa BSS,” ameongeza.

No comments:

Post a Comment