Tuesday 26 July 2016

Mahakama yamwachia huru staa wa Bollywood, Salman Khan

Muigizaji wa filamu nchini India, Salman Khan, ameachiliwa huru na mahakama moja kwa kosa la kumpiga risasi na kumuua mnyama wa mwituni aliye katika hatari ya kuangamia kabisa duniani.
Alikuwa ameshtakiwa kwa kuwaua swala watatu katika jimbo la Kaskazini la Rajasthan mwaka wa 1998. Mwaka uliopita aliachiliwa na mahakama kwa kosa jingine la kumkanyaga na kumuua mtu asiye na makazi.

Salman Khan, ni nyota wa filamu kutoka Bollywood, ambaye ana sifa ya kujikuta mashakani mara kwa mara. Mwaka 1998 alilaumiwa na kabila moja la Rajasthan kwa kupiga risasi na kuwaua swala watatu wakati alipokuwa katika shughuli za uwindaji.

Swala hao wanalindwa kisheria na pia wanasujudiwa na kabila lililoshtaki.

Alikuwa amepatikana na kosa na mahakama ya chini na kuhukumiwa kifungo lakini sasa ameachiliwa baada ya kukata rufaa.

No comments:

Post a Comment