Monday 25 July 2016

Mashabiki wazishtukia picha za Temba zinazomuonyesha amefunga ndoa


 Mashabiki wa muziki katika mitandao ya kijamii wazipokea kiutofauti picha zinazomuonyesha msanii wa muziki kutoka TKM Wanaume Family, Temba akiwa amefunga ndoa.




 Temba akiwa na mrembo kutoka Afrika Kusini.

Huwenda ikawa sio kweli kama mashabiki katika mitandao ya kijamii wanavyozungumza kutokana na rapper huyo kuonekana hivi karibuni akiwa na director Justin Campos wa Afrika Kusini.
Wiki moja iliyopita, Mkurugenzi wa TMK Wanaume Family, Mkubwa Fella alitoa taarifa kwa mashabiki wa muziki kwamba staa huyo anaelekea nchini Africa Kusini kuandaa kazi mpya.


 

Kupitia ukurasa wa instagram, msani wa kundi la TMK Wanaume Family Chege aliandika:

Naomba sana nisaidieni kumpa hongera amani james kwa jambo hili la kheri
HONGERA sana bro Temba.
Baada ya kauli hiyo, mashabiki katika mitandao ya kijamii wamekuwa na maoni tofauti juu wa picha hiyo.
Mwigane
_Jamani eeh? Uyu jamaa. Si” arishaoa? Au hiyo ni video ya wimbo?

Salehenemganga579

Kweli jamani alioaga uyu.duh nas anakipaji.tena alioaga kiti kama st joseph au st alban dah

Allie_kb


Hii ni nyimbo bila shaka maana @mhtemba alishaowa kipind cha nyuma

tathriba_

mmhhh watu hawataki kutoa kiki wameshtuka

No comments:

Post a Comment