Mgombea urais wa chama cha
Republican nchini Marekani Donald Trump amemsifu kiongozi wa zamani wa
Iraq Saddam Hussein akisema aliweza kukabiliana vyema na magaidi.
Bw
Trump alikuwa akihutubia mkutano wa kampeni eneo jimbo la North
Carolina Jumanne alioanza kuzungumza kuhusu kiongozi huyo aliyeuawa kwa
kunyongwa Desemba 2006.“Saddam Hussein alikuwa mbaya, kweli? … Lakini mnafahamu ni jambo gani aliweza kulifanya vyema sana? Aliwaua magaidi. Alifanya hivyo vyema sana,” Trump alisema.
“Hawakuwasomea haki zao, hawakunena lolote. Walikuwa magaidi, mambo yao kwisha.”
- Trump: Dunia ingekuwa bora na Gaddafi na Saddam
- Trump: Ninaweza kuzungumza na Kim Jong-un
Kabla ya uvamizi ulioongozwa na Marekani, ambapo Saddam aliondolewa madarakani, Iraq ilikuwa imeorodheshwa na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kama taifa linalofadhili ugaidi.
Amesema matamshi kama hayo yanaashiria “ni jinsi gani itakuwa hatari (kuwa na Trump) kuwa Amiri Jeshi Mkuu na jinsi ambavyo hafai kuhudumu kama rais.
No comments:
Post a Comment