Monday, 1 February 2016

1
Afisa Wanyamapori kutoka Wizara ya Mali Asili na Utalii Bw.Sadick Lotha akiwaeleza waandishi Wa Habari leo Jijini Dar es salaam kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Ardhi oevu Duniani inayotarajiwa kufanyika februari 2,2016 ambapo siku hiyo itatumika kutoa elimu kwa kuwakumbusha Watu kuhusu uhifadhi na Matumizi endelevu ya Rasilimali za ardhi oevu. Kulia ni Afisa Habari wa Wizara hiyo Bw. Lusungu Helela, kushoto ni Afisa Wanyamapori Mkuu na Mratibu Kitaifa wa Uhifadhi Ardhi Oevu Bw. Pellage Kauzeni.
2
Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Mali Asili na Utalii Bw. Pellage Kauzeni akitoa wito kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya ardhi oevu kushirikiana na Serikali katika kuyatunza maeneo hayo kushoto ni Afisa Wanyamapori kutoka Wizara ya Mali Asili na Utalii Bw.Sadick Lotha na kulia ni Afisa Habari wa wizara hiyo Bw. Lusungu Helela.
3
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatlia mkutano wa Wizara ya Mali Asili na Utalii uliolenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maadhimisho ya siku ya ardhioevu ambayo huzuia mmomonyoko wa udongo kwenye fukwe unaoweza kusababishwa na mawimbi ya bahari.

 
Na Mwandishi wetu
MKUU wa Wilaya ya Wete  Rashid Hadid Rashid amewataka walimu wakuu katika wilaya hiyo , kusimamia upatikanaji wa hati miliki ya maeneo ya skuli zao .
Amesema kuwa Maeneo mengi ya Skuli  ndani ya Wilaya ya Wete yanakabiliwa na migogoro ya Ardhi inayosababishwa na kutokuwepo na hati miliki .
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na walimu Wakuu wa Wilaya hiyo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Zamani wa Chuo cha uwalimu Benjamini Mkapa kwenye mkutano wa kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo  .
 ‘Kila mwalimu analojukumu la kusimamia upimaji wa maeneo ya Skuli na kisha kupatiwa hati miliki , hii itaondoa migogoro inayojitokeza kwa sasa ”alisisitiza
Amesema kwamba Serikali ya Wilaya iko tayari kushirikiana na Uongozi wa Skuli katika Wilaya hiyo kuhakikisha maeneo hayo yanapimwa na kupatiwa  hati miliki .
“Serikali ya Wilaya iko tayari wakati wowote kutoa msaada wa uoatikanaji wa hati miliki ya Maeneo ya Skuli , tunashirikiana kufuatilia katika ngazi zinazohusika ”aliafahamisha.
Mapema Afisa Elimu na Mafunz ya Amali Wilaya hiyo Khamis Said Hamad amesema kwamba yapo Baadhi ya maeneo ya Skuli yamepimwa lakini imekuwa ni vigumu kupatikana kwa hati miliki .
Hivyo Ameiomba Serikali ya Wilaya kusaidia kupatiokana hati miliki katika Skuli hizo ambazo tayari maeneo yake yamepimwa ikiwa skuli ya Sekondari ya Pandani .
“Zipo skuli tayari maeneo yake yamepimwa lakini bado hati miliki hazijapatikana , ikiwemo Skuli ya Sekondari ya Pandani ambayo eneo lake limeshapimwa ”alifahamisha.
Naye Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Sekondari ya Mchangamdogo Juma Said Hamad ameiomba Serikali ya Wilaya kulipa kipaumbele suala la kuyapima maeneo ya skuli .
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba asilimi 60 ya maeneo ya Skuli za Wilaya ya Wete hayana hati miliki jambo ambalo linasababisha maeneo hayo kuvamiwa na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na makaazi

No comments:

Post a Comment