Friday 25 August 2017

Venezuela yazifungia Televisheni mbili za Colombia

Venezuela imezifungia televisheni mbili kutoka nchini Colombia kurusha matangazo nchini humo.
Serikali ya Venezuela bado haijatoa sababu ya kufanya hivyo, lakini Rais Nicolas Maduro amewahi kuvituhumu baadhi ya vyombo vya habari vya Colombia kwa kuingilia mambo yake ya ndani.
Mmoja wa wamiliki wa televisheni hizo amesema anaamini zuio hilo limetokana na kuwasili nchini Colombia kwa Luisa Ortega ambaye amekuwa akimpinga Rais Maduro.

No comments:

Post a Comment