Thursday 31 August 2017

Marekani kuongeza askari Afghanistan

wizara ya ulinzi nchini Marekani Pentagon imethibitisha Kuhusu uwepo wa askari kumi na moja elfu wa Marekani hukoAfghanistan, hii ni Idadi kubwa zaidi kuliko elfu nane na mia nne, kinyume na ilivyoainishwa awali.
Maofisa wa ngazi za juu kutoka katika wizara hiyo wanasema takwimu hiyo mpya ni pamoja na vitengo vya muda na kubadilisha pamoja na majeshi ya kawaida.
Taarifa hiyo inafuatia wizara hiyo ya ulinzi ikijiandaa kupelaka Kama askari elfu nne zaidi nchini Afghanistan ili kusaidia kupambana na askari wa Taliban na kuwasaidia Afghanistan kujinyakulia ushindi na hii ni kwa muujibu wa sera mpya iliyotangazwa na Rais Trump wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment