Tuesday 29 August 2017

Haki za Binadamu waungana na mawakili

  Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini (LHRC) chaungana na wanachama wa TLS kulaani tukio la ofisi za IMMMA Advocates kupigwa bomu.
Kwamujibu wa Mkurugenzi wa Kituo hicho Hellen Kijjo Bisimba amesema hatua hiyo inaashira kuonesha kutoridhishwa na kitendo hicho na kwamba vyombo vya dola vinatakiwa kufanya uchunguzi wake kwa haraka na kutoa majibu yaliyosahihi.

Hata hivyo Rais wa TLS kwaniaba ya mawakili wenzie Tundu Lissu ameeleza kuwa hawataki kuona Tanzania ya Mabomu kwakuwa vitendo vya namna hiya na vile alivyoviita vya kikatili wamekuwa wakifanyiwa mawakili bila kujali kuwa wana ulinzi kisheria.

No comments:

Post a Comment