Sunday 27 August 2017

Marekani: Mafuriko mabaya yatokea baada ya janga la kimbunga Harvey

Gavana wa jimbo la Texas, Greg Abbott, anasema kuwa, mafuriko ya kutisha ndio swala lake kuu la msingi, huku mvua kubwa inayoandamana na kimbunga kiitwacho Harvey, ikiendelea kutatiza mambo katika jimbo hilo.
Bwana Abbott anasema kwamba, miji miwili katika barabara inakopitia kimbunga hicho, Houston na Corpus Christi, tayari imepokea mvua zaidi ya Sentimita 50 na kiwango kinatarajiwa kuongezeka kwa mita moja zaidi, kabla ya kimbunga hicho kupungua, ifikiapo katikati ya wiki hii.
Zaidi ya wafungwa 4,500 katika gereza moja kusini mwa Houston wamehamishiwa hadi gereza lingine mashariki mwa Texas kwa sababu ya kuongezeka kwa maji ya mto Brazos ulioko karibu.
Maafisa wakuu wa jimbo hilo wamesema.
Juhudi za uokoaji, zinatatizwa na upepo mkali.
Mamia kwa maelfu ya watu wamekatikiwa na guvu ya umeme.

Kufikia sasa kifo cha mtu mmoja tu kimethibitishwa kutokea katika mji wa Rockport, huku wakuu wakionya kuwepo kwa mafuriko zaidi ya maji.

No comments:

Post a Comment