Wednesday 23 August 2017

Habari Picha

PIC 1
Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni (katikati) akiongoza kikao wakati Wajumbe wa Kamati hiyo walipokutana na Wajumbe wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada  katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.
PIC 2
Mwenyekiti  wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada  Mhe. Yasmin Ratansi (wa kwanza kushoto) akisisitiza jambo wakati Wajumbe wa Chama hicho kutoka Canada walipokutana na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.
PIC 3
Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada ambae pia ni Mbunge, Mhe. Yasmin Ratansi akimkabidhi  zawadi Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni mara baada ya Wajumbe wa pande zote mbili kuzungumza mapema leo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
PIC 4
Wajumbe wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika picha ya pamoja na Wajumbe wa   Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada mara baada ya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
        Picha na Ofisi ya Bunge

No comments:

Post a Comment