Thursday 31 August 2017

Liverpool waibomoa Arsenal, wamnyakuwa Chamberlain

Hatimaye aliyekuwa mchezaji wa Arsenal, Alex Oxlade-Chamberlain amefanikiwa kusaini mkataba wa kujiunga na Liverpool.
Mchezaji huyo amejiunga na Majogoo hao wa Anfield kwa ada ya uhamisho wa paundi milioni 40.
Awali Chamberlain alikuwa akiwaniwa kwa ukaribu na Chelsea ambayo hakufanikiwa kuipata saini yake.
Hata hivyo mchezaji huyo amewashangaza mashabiki wengi baada ya kukataa kuongeza mkataba mpya na Arsenal ambao ungemfanya kuweza kulipwa kiasi cha paundi 180,000 kwa wiki na badala yake amekubali kujiunga na Liverpool kwa kulipwa mshahara wa paundi 120,000 kwa wiki.

No comments:

Post a Comment