Monday 31 July 2017

Al Shabaab waua wanajeshi 24

Wanajeshi 23 wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika (AMISOM) na askari mmoja wa Somalia wameuawa katika mtego wa kuvizia ulioandaliwa na wapiganaji wa Al Shabaab Kusini Magharibi mwa Somalia.
Mapigano yalizuka baada ya wanamgambo wa Al-Shabaab kuvamia vikosi vya AMISOM mapema Jumapili katika Wilaya ya Bulamareer ya Mkoa wa Lower Shabelle kilomita 140 Kusini Magharibi mwa mji wa Mogadishu.
"Tumechukua miili 23 ya askari waliouawa wa AMISOM na askari mmoja wa Somalia kutoka kwenye eneo ambalo Al Shabaab waliweka mtego wa kuvizia na kuvamia,” alisema Ali Nur, naibu gavana wa Lower Shabelle.

Wapiganaji hao wa Al Shabaab ambao wamekuwa wakipigana na majaeshi ya serikali ya Somalia inayoungwa mkono na nchi za Magharibi wamedai kwamba wameua askari 39 wa AMISOM.

No comments:

Post a Comment