Serikali imeanza hatua
za awali za kufanyia utafiti wa ubora wa picha zinazopigwa na ndege
isiyo na rubani katika matumizi ya kuandaa ramani.
Hadi sasa picha
zilizopigwa zinaonyesha kuwa nzuri ambapo mafunzo zaidi juu ya matumizi
ya picha hizo na jinsi ya kuandaa ramani yanahitajika.
Serikali ya Tanzania na
ile ya Korea Kusini zinaendelea na mazungumzo ili Korea iweze kutoa
mafunzo na ushauri wa kitaalam kuhusu matumizi ya drones katika kuchora
ramani na kuhuisha ramani za siku nyingi.
Kwa kuanzia utaangaliwa
uwezekano wa picha hizo kutumiwa kupanga ukuaji wa miji midogo kama
Kibaigwa, Uvinza, Chanika na mingineyo ili ikue kimpangilio.
No comments:
Post a Comment