Thursday 23 June 2016

Iceland yasonga Euro sasa kuivaa England

 
Taifa dogo kwa maana ya idadi ya watu, Iceland limeicharaza Austria kwa goli 2 - 1 katika mchuano wa soka wa Euro 2016, na kufuzu katika hatua ya 16 bora .

Iceland iliiadhibu Austria mabao mawili kwa moja na sasa watakutana na England. Mtangazaji wa mpira kutoka Iceland alishindwa kujizuia pale ambapo Arnor Ingvi alizitikisa nyavu katika dakika za majeruhi.
Wakati Mtangazaji wa Iceland amefurahi kweli kweli kwa Timu yake kufuzu, Mtangazaji Mreno yeye anaugulia maumivu ya moyo kwa tukio alilofanyiwa na Ronaldo na kumnyang'anya kipaza sauti na kukitupa mtoni.

No comments:

Post a Comment