Tuesday 26 September 2017

WhatsApp China yapatikana kwa Shida

China. Mtandao wa WhatsApp umeingia kifungoni nchini China ukiifuatia na Instagram, Twitter, Facebook, Gmail, Snapchat na Pinterest.
WhatsApp imeanza kufungiwa taratibu katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, kwa mujibu wa taasisi inayoratibu masuala ya mitandao duniani, Open Observatory of Network Interference (OONI).
Mtandao wa Shirika la Utangazaji CNN unaripoti kuwa katika miezi ya hivi karibuni WhatsApp imekuwa ikipatikana kwa shida.
Mtandao huo ulianza kufungiwa taratibu wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu wa chama tawala cha Communist, utakaoanza Oktoba 19 mwaka huu.
Kwa kawaida nchi hiyo hudhibiti matumizi ya mtandao katika kipindi cha uchaguzi mkuu ambao hufanyika kila baada ya miaka mitano.

China inatumia mtindo wa Great Firewall katika kudhibiti matumizi ya intaneti ambayo hujumisha sera na teknolojia.

No comments:

Post a Comment