Tuesday 26 September 2017

Mwigulu:Wananchi wawe na imani na vyombo vya ulinzi na usalama

  Image result for Mwigulu Nchemba
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amewataka wananchi nchini kuendelea kuwa na imani kubwa na vyombo vya ulinzi na usalama nchini katika kulinda Raia na mali zao
Waziri Mwigulu amesema kuwa kama yeye ndiye aliyepewa dhamana ya usalama wa Raia na mali zao katika wizara ya mambo ya ndani basi hapatatokea hata kakitongoji kamoja au kauchochoro ambacho kitaonekana kimeshindikana ndani ya nchi yetu, Ameyasema hayo akizungumza na wananchi wa kata ya Kinampanda wilaya ya Iramba mkoani Singida.
Waziri mwigulu ameongeza kuwa nchi hii ni nchi huru inajitegemea na kuna watu wanasema wanataka vyombo vya nje vifanye uchunguzi, hawa watu wanao fanya uhalifu nchini, upelelezi utafanywa na watu wetu, watakamatwa na vyombo vyetu na watafikishwa katika vyombo vya sheria vya hapahapa  tunatakiwa kuamini vyombo vyetu, kama serikali tutashugulikano kwelikweli na si kama hatujaanza nao tunashughulika nao

No comments:

Post a Comment