Friday 29 September 2017

Maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani

DSC_0817
Muakilishi wa Jimbo la Mpendae Said Mohd Dimwa wapili kushoto akifuatana na Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Maandamano ya maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani yaliofanyika katika Ofisi ya Jumuiya ya watu wenye maradhi yasioambukiza (ZNCDA)Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja
DSC_0827
Maandamano yalioongozwa na Bend ya Chipukizi yakielekea katika Ofisi ya Jumuia ya watu wenye maradhi yasioambukiza katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja
DSC_0837
Vikundi mbalimbali vya mazoezi vikishajiisha suala zima la ufanyaji mazoezi ili kulinda afya na maradhi mbalimbali, katika siku ya maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
DSC_0852
Makamo mwenyekiti wa ZNCDA Ali Zubeir Juma akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
DSC_0890
Mgeni rasmi katika maadimisho ya siku ya Moyo Duniani Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae Said Mohd Dimwa akitoa hotuba kuhusiana na kujikinga na maradhi mbalimbali yanayotokana na Ulaji,Unywaji wa Pombe na Uvutaji wa Tumbaku katika maadhimisho hayo yliofanyika katika Ofisi ya Jumuiya ya watu wenye maradhi yasioambukiza (ZNCDA)Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
DSC_0903
Wananchi mbalimbali waliojitokeza kupimwa afya zao katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment