Thursday 21 September 2017

Kimbunga Maria: Kisiwa chote cha Puerto Rico hakina umeme

Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5.
Abner Gómez, ambaye ni mkuu wa utoaji huduma za dharura alisema kuwqa hakuna mtu anayetumia umeme aliye na huduma hiyo kwa sasa.
Kituo cha vimbunga cha Marekani kinasema kuwa mafuriko makubwa yanaikumba nchi hyo, Maria kwa sasa kinaondoka nchini Puerto Rico na kumepunguza nguvu zake hadi kiwango cha pili
.

Baada ya kimbunga Maria kuipiga Puerto Rico, gavana ameamrisha watu kusalia manyumbani mwao kuanzia saa kumi na mbili jioni na hadi saa kumi na mbili asubuhi.
Hi ni hatua ya kuwazuia watu kupata ajali kutokana na nyaya za umeme zilizoanguka na vifuzi vilivyo barabara za mji.
Mapema Bw Rossello alimuomba Rais Donald Trumo kukitangaza kisiwa hicho kuwa eneo la janga baada ya kimbunga kusababisha mafuriko makubwa na upepo unaotishia maisha.

Alisema kuwa kuna uwezekano wa uharibu mkuwa licha ya vitisho 500 kubuniwa kuwalinda watu.
Kimbunga hicho tayari kimesababisha vifo vya watu 7 katika kisiwa cha Dominica ambacho kiliathiriwa vibaya siku ya Jumatatu.

No comments:

Post a Comment