Saturday 30 September 2017

Halmashauri ya Kinondoni yasaini mikataba ya shilingi bilioni 49.


 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Aron Kagurumjuri amesaini mikataba miwili ya ujenzi wa barabara mbele ya mstahiki meya Benjamini Sitta yenye thamani ya shilingi bilioni 49.
Katika miradi hiyo itakayohusisha barabara ya Makanya, kisiwani, tandale, simu2000 ,  Ubungo external, kilingowima ni muendelezo wa awamu ya pili na tatu ya miradi ya uendelezaji wa jiji hilo DMDP, 
Kwa upande wake Mstahiki meya Benjamini Sitta ameyataka makampuni hayo jenzi (Estim na China Civil Engenearing Corp)  kuzijenga barabara hizo kama walivyokubaliana kwa kuwa barabara hizo ni muhimu mpaka kwa manispaa ya za jirani ikiwemo ya Ilala.
Hata hivyo amewataka wananchi wa maeneo husika kuhakikisha wanaitunza miundombinu ya barabara hizo mara baada ya kukamilika.

No comments:

Post a Comment