Tuesday 26 September 2017

Mbeya City yapata Kocha mpya

Image result for Nsanzurwimo Ramadhan
Klabu ya Mbeya City imefikia makubaliano na Kocha Nsanzurwimo Ramadhani kuwa Kocha Mkuu kwa mkataba wa awali wa Msimu mmoja wa ligi kuu ya Vodacom inayoendelea.
Kocha Ramadhan ni raia wa Burundi na anatarajiwa kujiunga na timu hiyo huko kanda ya ziwa inakoendelea na michezo yake ya ligi kuu.
Kocha Ramadhani amewahi kuwa kocha kwa nyakati tofauti katika vilabu mbalimbali nchini Burundi, Rwanda, Botswana, Malawi, Uganda, na Afrika ya Kusini, pia amewahi kuwa mshauri wa ufundi katika timu ya taifa ya Burundi na kocha msaidizi/kocha mkuu wa muda(caretaker) kwa timu ya taifa ya Malawi.
Imetolewa na
Shah Mjanja
Afisa Habari
MCCFC
0717282217

No comments:

Post a Comment