Amani ni msingi wa maendeleo na
hivyo ni muhimu kwa nchi yoyote duniani.Bila amani,nchi haiwezi kufanya
shughuli za maendeleo hata pale ambapo maendeleo
yameshapatikana,yanaweza kuvurugwa endapo amani itatoweke katika nchi.
Nchi ambazo kwa miaka ya hivi
karibuni zimejitahidi kupiga hatua za maendeleo na zinaendelea kufanya
jitiada kuhakikisha kuwa zinapiga hatua kubwa zaidi ya maendeleo kwa
faida ya wananchi wote,jitiada hizo pia,kwa baadhi ya nchi zimeathiriwa
na migogoro.
Matokeo ya migogoro hiyo ni
mamilioni ya waafrika wasio na hatia kupoteza maisha yao na mamilioni
zaidi kujeruhiwa.Pia mamilioni ya wanawake na watoto kupatwa shida kubwa
na baadhi ya watu kukimbia nchi zao na kukimbilia nchi za jirani katika
kuokoa maisha yao hivyo kujikuta wakiishi maisha ya dhiki nje ya nchi
yao.
Takwimu zinaonyesha kuwa mwaka
2009,Afrika ilikuwa na wakimbizi milioni 3 ambayo ni asilimia 20 ya
wakimbizi wapatao milioni 10.5 duniani.Aidha,Afrika inakisiwa kuwa ina
watu milioni kumi na mojana laki sita ambao wamelezimika kuhama makazi
yao kwa ajili ya vita
Migogoro migogoro huwa kikwazo
kikubwa cha shughuli za maendeleo siyo tu kwa watu binafsi bali pia kwa
taifa.Fedha ambazo zingeweza kuelekezwa kwenye huduma muhimu ya jamii
kama afya,elimu,maji ni fedha ambazo huelekezwa katika manunuzi ya
silaa.
Inakadiriwa kuwa hasara ya kiuchumi inakadiriwa kuwa wastani wa dola bilioni kumi na nane kwa kila mwaka sababu ya migogoro.
Hali hii ya migogoro katika bara
la Afrika imelifanya bara hili kujulikana kama bara la mapigano jambo
ambalo ni dhahiri linasikitisha hivyo hatuna budi kuondokana na hali
hiyo ya migogoro na kuwa bara huru lisilo na migogoro.
Ni kweli kuwa katika miaka ya
hivi karibuni kumekuwa na mabadiliko,kutokana na juhudi
zilizofanyika,Afrika imefanikiwa kupunguza idadi ya migogoro kuliko
ilivyokuwa katika miaka ya 1980 wakati ambapo nchi nyingi zilikuwa na
migogoro
Mfano nhci kama Liberia,Sierra
Leone,Msumbiji,Angolo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),Burundi na
Comoro nazo zimeendelea kuimarisha amani,Hali hii inatupa faraja lakini
bado Bara la Afrika linamigogoro kama vile ya Somalia na Darfur kuko
Sudani.
Mgogoro wa Somalia ni mgogoro wa
muda mrefu sasa ambao ni changamoto kubwa kwa bara la Afrika na jamii ya
Kimataifa kwa ujumla na hivyo unahitaji kuangaliwa kwa umakini zaidi.
Hali ya usalama nchini Somalia
ambayo kwa takribani miaka ishirini sasa imekuwa katika mazingira ya
kusikitisha kwa takribani miaka ishirini sasa imekuwa katika mazingira
ya kusikitisha ambapo kwa ujumla usalama wa wananchi wan chi hiyo umo
katika hali ya hatihati.
Kwa upande Tanzania tunafahari
kubwa ya kuwa mstari wa mbele katika kujenga mazingira yetu wenyewe ya
kuwa na amani,utulivu na mshikamano na pia katika kusaidia ndugu na
majirani zetu na sehemu nyingine za Bara la Afrika katika kufanukisha
lengo la kuleta amani popote pale inapokosekana.
Sote tunatambua kuwa Serikali ya
Tanzania katika kutetea amani katika bara la Afrika imepeleka vijana wa
Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) katika miaka ya nyuma walikwenda
nchini Liberia kwa lengo hilo.Na hivi karibuni wanajeshi wetu wamekwenda
Darfur kuungana na wanajeshi wengine wa Kiafrika na nchi nyingine chini
ya uongozi wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa.
No comments:
Post a Comment