Thursday 14 May 2015

Wananchi wa MATEMANGA wanaishi kwa hofu ya kuliwa na Simba wanaosumbua katika kijiji hicho.

Wananchi katika kijiji cha MATEMANGA wilayani tunduru mkoani RUVUMA wanaishi kwa hofu na kulazimika kutotembea usiku wakihofia kuliwa na simba wanaosumbua katika kijiji hicho  wakidaiwa kutoroka katika hifadhi ya taifa ya  SELOU  ambapo  mpaka sasa wameshakula mbuzi  zaidi ya ishirini.
Wamesema simba hao wanaodaiwa kuwa watatu na wazee ambao ina daiwa wametoroka porini baada ya kushindwa kuwinda kutokana na uzee ambapo wameshakula mbuzi zaidi ya ishirini kijijini hapo  wamekuwa wakisumbua katika kijiji hicho nyakati za usiku  na kuwafanya waishi kwa hofu  wakihofia kuliwa na simba hao.
Mhifadhi wa wanyamapori katika wilaya ya tunduru Bw.Charles Shawa  anasema kuwa msako mkali wa kusaka simba unaendelea huku akisema ni simba mmoja  tu ndiye  anayesumbua  kijijini hapo.
Mkuu wa wilaya ya tunduru Bw.Chande Bakary Nalicho anasema nguvu zimeongezwa katika msako wa simba  ambapo kuna askari wanyamapori sita katika  msako wa simba.

No comments:

Post a Comment