Wednesday 20 May 2015

Bodaboda walalamikia Polisi.


Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova

Waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda zaidi ya 50 wa jijini Dar es Salaam wameandamana hadi katika ofisi za gazeti hili kulalamikia unyanyasaji wanaofanyiwa na polisi jamii. 
Bodaboda hao kutoka maeneo ya Tanki bovu, Kawe na Mwenge wanadai kuwa wamechoshwa na unyanyasaji wanaofanyiwa na polisi jamii ambao wamekuwa wakiwakamata ovyo katika maeneo mbalimbali ya Jiji.
Kalos Meltus, alisema wamekuwa wakikamatwa na kutozwa faini kati ya Sh. 30,000 na 100,00 kila wanapoingia katikati ya Jiji na kudai kuwa wamegeuzwa mtaji wa baadhi ya viongozi kujipatia pesa.
Naye Erasto Matheo, alisema kuwakamata bodaboda katikati ya Jiji kunawaathiri kiuchumi kwa sababu wateja wao wengi wanakwenda mjini hivyo kuendelea kuwazuia ni kuwapa wakati mgumu kimaisha.
“Sababu inayotolewa kwamba sisi watu wa bodaboda tunashiriki vitendo vya uhalifu siyo kweli kwani licha ya kwamba tumekatazwa bado uhalifu unafanyika katikati ya Jiji,” alise

No comments:

Post a Comment