Tuesday 19 May 2015

Tanzania yamshikilia muasi wa ADF

Polisi nchini Tanzania wamethibitisha kuendelea kumshikilia Jamil Mukulu ambaye ni kiongozi wa waasi wa ADF wa Uganda. Mukulu anayekabiliwa na tuhuma kadhaa ikiwemo mauaji amefikishwa mahakamani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuandaa utaratibu wa kumrudisha Uganda ili akashtakiwe rasmi huko. Kiongozi huyo na kundi lake la ADF wanadaiwa kuhusika na uhalifu katika nchi za Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Mahakama imempa hadi tarehe 22 mwezi huu kuwasilisha pingamizi lake au la atarejeshwa Uganda. Mwandishi wetu Kulthum Maabad amezungumza na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini Tanzania, Diwani Athuman kuhusu hatua hiyo

No comments:

Post a Comment