Monday, 5 June 2017

Balozi Cisco Mtiro amefariki dunia

Mkuu wa Itifaki mstaafu Balozi Cisco Mtiro amefariki dunia katika Hospitali ya Aga Khan  jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Cisco Mtiro alikuwa Balozi wa Tanzania nchi za Malaysia, Phillipines, Cambodia, Singapore na Laos.
Kwa mujibu wa familia yake, msiba upo nyumbani kwa marehemu Mikocheni B jijini Dar es salaam ambapo Taratibu za mazishi zinaendelea

No comments:

Post a Comment