Wednesday 28 June 2017

Arsenal kumnua Arda Turan

 Klabu ya Barcelona imetangaza dau kwa klabu yoyote itakayohitaji kumnunua kiungo wao, Arda Turan, huku Arsenal ndiyo wakiwa mstari wa mbele kusaka huduma ya mchezaji huyo.
Mturuki huyo anaonekana kuimarika kiwango chake jambo linalomfanya aweze kuuzika klabuni hapo.
Nyota huyo amekuwa akikosa namba ya kikosi cha kwanza licha ya kiwango chake cha kuvutia na amefanikiwa kufunga mabao 13 katika mechi zote alizocheza msimu ulioisha.
Dau la Turan limetajwa kuwa ni Pauni 65 milioni na iwapo hatauzika msimu huu, huenda thamani yake ikashuka zaidi kutokana na kutimiza miaka 30 sasa.

No comments:

Post a Comment