Friday 23 June 2017

Kikao cha kuboresha Mahusiano kati ya TEMESA na wadau

unnamed
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu (katikati) akiongea na wadau (hawapo pichani) katika kikao cha wadau hao  kilichojadili namna bora ya kuboresha mahusiano kati ya TEMESA na wadau hao kilichofanyika  katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam, Kikao hicho ni maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko na kushoto ni Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo Bw. Slylivester Semfukwe
1
Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo Bw. Sylivester Semfukwe kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) akitoa ufafanuzi kutoka kwa wadau (hawapo pichani) ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini, wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu.
2
MSTAHIKI MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko akichangia mada katika Kikao  kilichojadili namna bora ya kuboresha mahusiano kati ya TEMESA na wadau hao kilichofanyika katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam, Kikao hicho ni Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini.
3
Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Hans Lyimo akiongea katika Kikao cha kujadili namna bora ya kuboresha mahusiano kati yao na TEMESA kilichofanyika katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam ikiwa ni Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini, wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko Japhet Maselle.
4
Mdau wa TEMESA akitoa maoni katika  Kikao  kilichojadili namna bora ya kuboresha mahusiano kati ya TEMESA na wadau hao kilichofanyika katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam ikiwa ni Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini.
5
Mwanasheria Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Gatian Mali akitoa ufafanuzi wa Kisheria kwa wadau (hawapo pichani) katika kikao cha kuboresha mahusiano ya pande mbili ikiwa ni Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam.
6
Baadhi ya Wadau wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakiwa katika picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dk. Mussa Mgwatu (watatu kutoka kulia waliokaa) mara baada ya kikao cha kuboresha mahusiano kati ya TEMESA na wadau hao kilichofanyika  katika ukumbi wa MT Depot jijini Dar es Salaam, Kikao hicho ni Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini

No comments:

Post a Comment