Tuesday, 20 September 2016

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi Mhe.George Simba Chawene amefanya ziara shule ya sekondari ya Ihungo ambayo imeathiriwa vibaya na Tetemeko la Ardhi.

ger1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi  Mhe.George Simba Chawene akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kutembelea shule ya sekondari ya Ihungo ambayo imeathiriwa vibaya na Tetemeko la Ardhi.Kushoto kwake ni Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama.
ger2
Wafanyakazi wa VETA wakiendelea na ubomoaji wa Shule ya Ihungo ambayo  inavunjwa na kujengwa upya kwa msaada wadau na Serikali baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi la hivi karibuni Mkoani Kagera.
ger3
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi  Mhe.George Simba Chawene akizungumza jambo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako mara baada  ya kutembelea shule ya sekondari ya Ihungo ambayo imeathiriwa vibaya na Tetemeko la Ardhi.
ger4
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akizungumza na wahandishi wa habari kuhusu hatua ambayo serikali imechukua kusaidia ukarabati wa shule ya Ihungo ambayo imeathiriwa vibaya na Tetemeko la Ardhi.KUlia kwake ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi  Mhe.George Simba Chawene

No comments:

Post a Comment