Monday 26 September 2016

Majina ya wasanii wengine watakaotumbuiza kwenye MTV MAMA 2016 yatajwa

Majina mengine ya wasanii wanaotarajiwa kuwasha moto kwa kutumbuiza kwenye jukwaa la tuzo za MTV MAMA 2016 yametajwa.
Wasanii waliotajwa kwenye orodha hiyo ni pamoja na Diamond Platnumz (Tanzania), Patoranking (Nigeria) Kwesta (Afrika kusini) na Emtee (Afrika Kusini).

Wasanii wengine ambao wanatarajiwa kutumbuiza siku hiyo ni pamoja na Yemi Alade, Alikiba, Ycee, Cassper Nyovest, Babes Wodumo na Nasty C.

Tuzo hizo zitafanyika October 22, 2016, kwenye ukumbi wa Ticket Pro Dome, Johannesburg, Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment