Wednesday 28 September 2016

Michezo ya watumishi wa Serikali kutoka katika Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa (SHIMIWI) itafanyika Mjini Dodoma

mo
Michezo inayowakutanisha watumishi wa Serikali kutoka katika Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa (SHIMIWI) itafanyika Mjini Dodoma kuanzia tarehe 14 – 27 Oktoba, 2016 katika viwanja vya Jamhuri, Chuo Kikuu Huria, Don Bosco, Chuo kikuu cha St.Jones, Magereza na Shule za Sekondari za Jamhuri, Central na Dodoma.
Michezo itakayoshindaniwa ni: Mpira wa Miguu, Netiboli, Kuvuta Kamba, Riadha, Baiskeli, Karata, Bao, Drafti na Darts.
Ratiba ya Michezo ya ufunguzi ; Mpira wa Miguu – Wizara ya Elimu itakutana na Ofisi ya Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali, Netboli- Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma itacheza na RAS- Manyara, Kuvuta Kamba Wanaume – Ofisi ya Rais – Ikulu watavutana na Ofisi ya Bunge na Kamba wanawake RAS Iringa watavutana na Wizara ya Afya. 
 
          Kabla ya Michezo hiyo asubuhi itatanguliwa na Ibada maalum itakayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri ya kumwombea Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere pia kumtakia afya njema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na wasaidizi wake katika kuliongoza Taifa letu kwa mafanikio, baada ya tukio hilo Kutakua na zoezi la kupanda Miti. Nawakaribisha Wakazi wote wa Dodoma kujitokeza kwa wingi katika viwanja vilivyotajwa hapo juu ili kupata burudani. Hakutakuwa na kiingilio.
      Aidha, naviomba Vilabu kukamilisha taratibu za usajili mapema iwezekanavyo kama ilivyoelekezwa awali.
 
Moshi Y. Makuka
KAIMU KATIBU MKUU – SHIMIWI.
Imetolewa leo tarehe 28 Septemba, 2016

No comments:

Post a Comment