Saturday 24 September 2016

Vanessa na Trey songz kuja na Collabo ya pamoja

Ni Headlines za Vanessa Mdee ambae amekuwa ni moja kati ya wasanii wa Africa waliochaguliwa kurekodi wimbo na mshindi wa Grammy na mwimbaji wa RNB nchini Marekani,

Trey Songz kupitia msimu wa 4 kipindi cha Coke Studio Africa.Akizungumza na lindiyetu.com Vanessa Mdee aliyaongea haya, "Niko Kenya nikifanya msimu wa Coke Studio Africa ambapo msimu huu tumemkaribisha msanii wa kimarekani Trey Songz kuja kufanya collaboration na waafrika nikiwemo na mimi" "Ni experience ya kipekee sana nimefuraha sana kuwa katika nafasi hii ya kufanya collabo nae kwani ni hatua nzuri kwangu pia kuitangaza nchini yangu"Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza Vanessa Mdee akielezea collabo yake na Trey Songz.

No comments:

Post a Comment