
Pluijm, ambaye mara nyingi hapendi kumzungumzia mchezaji mmoja mmoja kwenye kikosi chake, lakini mwishoni mwa wiki alishindwa kujizuia na kudai kuwa Mahadhi amekuwa akicheza kwa kasi, na kuhaha uwanjani huku na kule kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.

“Mahadhi kwangu ni ‘Super Sub’ washambuliaji wangu walipoteza nafasi nyingi na walikosa umakini, lakini alipoingia Mahadhi alibadili mchezo, alicheza kwa kasi na kupeleka mashambulizi zaidi kwa wapinzani ndio uchezaji ninaouhitaji,”alisema Pluijm huku akiangua kicheko cha furaha.
Pluijm alisema aina ya uchezaji wa Mahadhi, inamshawishi kocha kumpa nafasi ya kucheza hata kama imebaki dakika moja kabla ya mchezo kumalizika.
No comments:
Post a Comment