
Hayo ni kwa mjibu wa maafisa wakuu katika jimbo hilo.
Gavana wa jimbo hilo Bismillah Afghanmal, amesema kuwa basi hilo lilikuwa njiani kuelekea Kabul kutoka Kandahar, lilipogongana na tangi hilo la mafuta na kushika moto. Baadhi ya watu walichomeka kiasi cha kutotambuliwa.
Polisi wamesema baadhi ya majeruhi wamepelekwa katika hospitali kadhaa katika makao makuu ya jimbo la Qalat, na pia katika jimbo jirani la Kandahar.
No comments:
Post a Comment