Sunday 27 March 2016

Wafanyakazi wa TBL Arusha Washiriki Uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza


12Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL cha Arusha wakifanya mazoezi ya kukimbia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza mwishoni  mwa wiki
345
7Meneja wa kiwanda cha TBL mkoa wa Arusha,Salvatory Rweyemamu akipiga mpira kuashiria kuanzishwa kwa kampeni ya Afya Kwanza iliyoanzishwa na TBL Group kwa lengo la kuimarisha afya za wafanyakazi wake.
6   Meneja Uendeshaji wa taasisi ya AAR Insurance Tanzania Ltd, Dk Harold Adamson akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha TBL mkoa wa Arusha juu ya umuhimu wa kuimarisha afya zao kwa kufanya mazoezi wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza uliofanyika kiwandani hapo mwishoni mwa wiki.8Wafanyakazi wa TBL kiwanda cha Arusha wakimsikiliza mtaalamu wa lishe huku wakijipatia matunda  baada ya kufanya mazoezi ya kuimarisha viungo vyao wakati  wa uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza iliyofanyika kwenye kiwanda hicho eneo la Themi jijini Arusha mwishoni mwa wiki.
Kampeni ya TBL Group imezindua kampeni ya kuimarisha afya za wafanyakazi wake wote ambapo wanashiriki kufanya mazoezi ya mwili sambamba na  kupatiwa  kupatiwa elimu inayohusiana na lishe bora na matumizi ya vyakula visivyo na athari.
Afya Kwanza ambayo imeanzia kwa wafanyakazi waliopo Makao makuu na viwanda vilivyopo jijini Dar es Salaam Mwishoni mwa wiki imezinduliwa katika kiwanda cha Arusha na kushirikisha wafanyakazi wa kiwanda hicho.
Msimamizi wa Programu hii ,Julieth Mgani alisema kuwa itakuwa endelevu na wafanyakazi wameonekana kuifurahia katika kipindi cha muda mfupi tangia ianzishwe.

MBIO ZA MAGARI ZA VAISAKH RALLY 2016 ZINAFANYIKA JUMAPILI HII VIWANJA VYA KIA,KILIMANJARO

Mratibu wa Mashindano ya Mbio za Magari ya Vaisakh Rally 2016 ,Faheem Aloo akiwa na Mwenyekiti wa matukio wa klabu ya Kilimanjaro Motorspot ,Juma Shaaban.
Mratibu wa Mashindano ya Mbio za Magari ya Vaisakh Rally 2016 ,Faheem Alooakizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani ) kuhusu maandalizi ya Mbio za Vaisakh Rally 2016 zinazofanyika Jumapili hii katika viwanja vya KIA.
Zawadi kwa washindi.
Hari Singh Rally Team ni moja ya madereva walioingiza gari mpya aina ya Subaru za mwaka 2015 katika mashindano hayo.
Jamil Khan ataongoza team Evolution katika mashindano hayo.
Raia wa Italiano Piero Canobbio ni mmoja wa madereva ambao wanatajwa kuwa tishio katika mbio hizo ambaye anashiriki kwa mara ya kwanza akitokea nchini Kenya.
Magari ya Mashindano yakijipanga kwa ajili ya ukaguzi wa mwisho .
Gurjit Dhan Dereva anayepewa nafasi kubwa ya kufanya vyema katika mashindano hayo.
Dereva Larry Horn anaingia katika mashindano hayo akiwa na gari aina ya Porche.
Baadhi ya magari yanayoshiriki mashindano hayo yanayofanyika Jumapili hii katika viwanja vya KIA,
 

No comments:

Post a Comment