Wednesday 30 March 2016

Millioni 37 Zatengwa Kukarabati Barabara ya kata ya Pazuo/Mkuranga


Na Chrispino Mpinge
JUMLA ya Sh Milioni 37 zimetangwa kwa ajili ya kukarabati
barabara ya Mbogo na Mbezi Muungwana, inayopita katika vijiji kadhaa vya Kata
ya Panzuo, wilaya Mkuranga, mkoani Pwani kwa ajili ya kupunguza adha za ubovu
wa barabara wanazokutana nazo wananchi wa maeneo hayo hali inayopelekea wakati
mwingine akina mama kujifungulia njiani.
Mwendesha bodaboda Ramadhan Rajab akijaribu kupita katika barabara mbovu inayotokea Kimanzichana kuelekea vijiji vya Mnyonzole na Kibesa, Kata ya Panzuo, wilayani Mkuranga, mkoani Pwani.
 
Mapema mwezi uliopita baadhi ya wananchi wakiwamo akina mama
Walizungumza kwa uchungu juu ya ukosefu wa barabara katika maeneo hayo, jambo
linalowanyima raha na ukosefu wa mbinu za kujikwamua kiuchumi kwa kukosekana
barabara inayopitika kwa wakati.
 
Akizungumza juu ya ukosefu wa barabara na mipango yao,
Diwani wa Kata ya Panzuo, wilaya Mkuranga, mkoani Pwani, Juma Magaila, alisema
kwamba kiasi hicho cha pesa kitaanzia kwanza kuweka kifusi katika maeneo
Mbalimbali ili wananchi wae ndelee na majukumu yao kwa kuhakikisha kwamba suala
hilo la barabara mbovu linashughulikiwa.
 
Alisema ni kweli wananchi katika maeneo hayo wamekuwa
wakiishi kwa mashaka hususan mvua zinapoanza kunyesha, ila tayari fedha
zimetangwa kwa ajili ya kuanza ukarabati wa barabara hiyo inayotumiwa na
wananchi wengi wilayani Mkuranga.
 
“Tunaendeelea na mikakati ya kuikwamua Kata yetu hususan
katika changamoto kubwa za ubovu wa barabara wanazokutana nazo wananchi wangu
Wa Panzuo ambao wanashindwa kukuza uchumi wao kwasababu barabara haipitiki
kirahisi wakati wote.
 
“Naamini kwa kutengwa kiasi cha Sh Milioni 37 kutachangia
kwa kiasi kikubwa kuiweka barabara yetu katika kiwango cha kupitika huku
Tukielekea katika safari ya kuona tunafikia hatua ya kuiwekea changarawe na
mengineyo,” Alisema.
 
Awali wananchi wa vijiji vya Kibesa wakiongozwa na
Mwenyekiti wao Khamis Ningwe walitumia muda mwingi kuilalamikia barabara hiyo
Sanjari na kuiomba serikali ya Halmashauri ya wilaya Mkuranga iliangalie suala
hilo kwa jicho pevu.
Endapo barabara hiyo itakarabatiwa japo kwa kiwango cha
kifusi, si tu akina mama wajawazito hawatajifungulia njiani kunaponyesha mvua,
Bali wananchi wanaweza kuingiza kipato kwa kuuza bidhaa zao mbalimbali kama
Vile nanasi na nyinginezo zinazopatikana katika maeneo hayo sanjari na kuleta
urahisi watu kuingia na kutoka kwenye maeneo hayo.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAENDELEO YA MIUNDOMBINU,YAFANYA ZIARA YATEMBELEA MRADI WA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA (JNIA)

 KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu, imefanya ziara ya kutembelea mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Terminal Three- TBIII), jijini Dar es Salaam, Machi 29, 2016 ambapo awali wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Profesa Norman Adamson Sigalla King, walipatiwa maelezo ya kina ya maendeleo ya mradi huo unaohusisha jengo la kisasa la abiria na sehemu ya kuegesha ndege kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria na sehemu ya maegesho ya magari. Baada ya maelezo hayo ya kina yaliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini, (TAA), Mhandisi George Sambali akisaidiana na baadhi ya wakurugenzi wengine wa Mamlaka hiyo, wajumbe hao walitembelea mradi huo na kujionea hatua mbalimbali za ujenzi ambapo kwa sasa ujenzi umefikia karibu asilimia 60. Pichani, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Mhandisi George Sambali, (kushoto), akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Norman Adamson Sigalla King, (kulia), na baadhi ya wajumbe na maafisa wa TAA
 Mwenyekiti wa Kamati, akizungumza
 Kaimu Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA), Paul Rwegasha, akizungumza na wajumbe wa Kamati hiyo ya Bunge kabla ya kutembelea mradi
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo na maafisa wa TAA, wakisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Mhandisi George Sambali (hayupo pichani)
 Mkurugenzi wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed Millanga, (kulia), akitoa maelezo ya maeneleo ya mradi huo. (kushoto) ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa TAA, Laurent Mwigune
 Mjumbe wa Kamati, Anna Richard Lupembe, akizungumza
 Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu, na Mbunge wa Fuoni, Zanzibar, Abbas Ali Hassan Mwinyi, (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa TAA, Ramadhan Maleta, na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Laurent Mwigune (kushoto)
 Mkurugenzi wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed Millanga(kushoto), akimueleza Mwenyekiti wa Kamati, Profesa Sigalla, sehemu ya maegesho ya ndege
 Mkurugenzi wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed
Millanga(kushoto), akimueleza Mwenyekiti wa Kamati, Profesa Sigalla,
(kulia kwake) na baadhi ya wajumbe na maafisa wa TAA, wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Sambali, (wakwanza kulia), sehemu ya maegesho ya ndege
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania, ATCL, Johnson Mfinanga akizungumzia hali ya shirika hilo
 Afisa Mkuu wa Masoko wa TAA, Scholastica Mukanjanga, akizungumza
 Mjumbe wa Kamati akizungumza
 Mjumbe wa Kamati akizungumza
 Mjumbe wa Kamati, Abass Ali Hassan Mwinyi, (katikati), akizungumza
Sehemu ya jengo la uwanja huo

No comments:

Post a Comment