Thursday 23 April 2015

Dk. Bilal: Umaskini sababu ya uharibifu wa mazingira.



Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema uharibifu wa mazingira katika nchi zinazoendelea ni kati ya sababu zinazofanya nchi hizo ziendelee kuwa maskini.
 
Dk. Bilal aliyasema hayo jana, jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa ripoti ya pili ya hali ya mazingira nchini nchini ya mwaka 2004, iliyoandaliwa na Wizara ya Mazingira.
 
Alisema upo uhusiano mkubwa kati ya mazingira na umskini kwa maana ya kwamba uharibifu wa mazingira unachangia kuongezeka kwa umaskini na kwamba kadri hali ya umaskini inavyoongezeka inasababisha uharibifu wa mazingira.
 
“Kwa maana hiyo umuhimu wa kulinda na kuhifadhi mazingira nchini unachochewa zaidi na ukweli kwamba mazingira ni mhimili wa sekta za uzalishaji kama vile kilimo, utalii, uvuvi na madini,” alisema na kuongeza:
 
“Changamoto iliyopo ni kuhakikisha mazingira na maliasili zetu zinatumika katika njia endelevu kwa kuzingatia uwiano mzuri kati ya matumizi ya maliasili, hifadhi zake na uwezo wake kuendelea kutoa huduma tunazozipata.”
 
Dk. Bilal alisema ili kusimamia masuala ya hifadhi ya mazingira kwa ufanisi ni lazima kudhibiti shughuli za binadamu zinazoathiri mazingira, masuala ya kijamii na kiuchumi kama vile ongezeko la watu, shughuli za kiuchumi zinazoendana na matumizi yasiyoendelevu ya mazingira zinazoweka shinikizo kubwa katika mazingira na kusababisha uharibifu.
 
Aidha, Makamu wa Rais alizitaka mamlaka za usimamizi kuhakikisha sheria, kanuni, mipango na programu mbalimbali zinazoandaliwa zinasimamiwa na kufuatiliwa kwa juhudi zote.
 
Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Binilith Mahenge, alisema pamoja na jitihada za kukabiliana na uharibifu wa mazingira, hali imeendelea kutoridhisha na kuwa takribani hekta 400,000 za misitu zinapotea kila mwaka huku takwimu za uchomaji moto ovyo kwa kipindi cha mwaka 2000 hadi 2011 kumekuwa na matukio 1,123,000 katika mikoa ya Rukwa, Kigoma, Tabora, Mbeya,

No comments:

Post a Comment