Sunday 30 April 2017

Mbeya City Yapata Mdhamini Wa Vifaa Vya Michezo

 Mfano wa Vifaa vya michezo vitakavyotumiwa na Timu ya Mbeya City kuanzia msimu ujao.

 Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda akisaini mkataba wa makubalino na uongozi wa Kampuni ya Sports Master chini yake Fadhili Nsemwa (kulia).

Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda (kushoto) akipokea mkataba kutoka kwa Kiongozi wa Sports Master ambao ni wadhamini wapya watakaosimamia maswala yote ya vifaa vya michezo vya Timu hiyo, Fadhili Nsemwa, baada ya kusainiana makubaliano.
Timu ya soka ya Mbeya City imepata mfadhili mpya wa timu hiyo ambaye atakuwa anasimamia maswala yote ya vifaa vya michezo ikiwemo jezi zote za timu hiyo zitakazotumiwa na wachezaji na zile za mashabiki kuanzia mwezi wa saba mwaka huu. Viongozi hao wamesaini mkataba wa udhamini huo uliofanyika katika ukumbi mdogo wa hoteli ya Mbeya Hill View kwa kuwaalika wadau wa mbeya city na vyombo vyote vya habari.

No comments:

Post a Comment