Wednesday, 5 October 2016

Taarifa ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto

tanzania
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali itahadhimisha siku ya Kimataifa ya Mtoto wa kike ili kutekeleza Azimio la Umoja wa Mataifa lililopitishwa mwezi Desemba mwaka 2011 likizitaka nchi wanachama kuadhimisha siku hii kupinga ndoa za utotoni.
Maadhimio haya yatafanyika kitaifa katika Mkoa wa Shinyanga kuanzia tarehe 5 Oktoba, 2016 na kilele chake kitakuwa tarehe 11/10/2016.  Maadhimisho haya ni moja kati ya jitihada za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa kutetea haki za mtoto wa kike na kufanya tathimini ya changamoto mbalimbali zinazomkabili mtoto wa kike.
Aidha Umoja wa Mataifa umetenga siku hii kwa lengo la kutafakari uzingatiaji wa haki na ustawi wa mtoto wa kike; na hivyo kuweka mipango thabiti ya kuboresha maisha yao na kuwawezesha kupata haki ya kulindwa, kuendelezwa, kuishi, kushirikishwa na kutobaguliwa katika familia na jamii zao. 
 
Wizara ya Afya, Maendeleleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inatoa wito kushirikisha wananchi na wadau wengine katika kuadhimisha siku hii, ili kupata ufahamu wa athari za ndoa za utotoni, na kuzingatia kuwarithisha wasichana maadili mema na maarifa ili kuwa na taifa lenye raia wema walioandaliwa kudumisha uzalendo, amani, uadilifu, uaminifu, kujiamini, na kutoa mchango katika maendeleo ya Taifa.
Kila mwaka, Maadhimisho haya huwa yanabeba Kauli Mbiu yenye ujumbe mahsusi. Kwa mwaka 2016 Kaulimbiu inasema “Mimba na Ndoa za Utotoni Zinaepukika Chukua Hatua Kumlinda Mtoto wa Kike’. Kaulimbiu hii inahimiza wazazi, walezi na jamii kutafakari na kuwekeza zaidi katika elimu ya mtoto wa kike ili kuwajengea uwezo wa kuwa na mchango katika familia na taifa kwa ujumla.
Aidha mgeni rasmi katika Maadhimisho haya ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb.).

No comments:

Post a Comment