Rais Magufuli aridhishwa na ujenzi wa mabweni UDSM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amehidi
kumalizia kiasi cha shilingi bilioni tano alichoahidi katika ujenzi wa
mabweni ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na kuahidi ajira
kwa watendaji wa ujenzi huo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake katika eneo la
Mlimani City ambapo kunafanyika ujenzi wa mabweni hayo ambapo amesema
amefurahi kuona kuwa wakandarasi wa ndani wakijenga kwa gharama nafuu na
kuwa kukamilika kwa ujenzi huo kutasaidia kuhifadhi wanafunzi zaidi ya
4000.
Kwa upande mwingine Dkt. Magufulli ameipongeza Wakala ya Majengo
Tanzania (TBA) ambao ni wakandarasi wa ujenzi huo kwa kukubali kujenga
mabweni hayo kwa gharama ya bilioni kumi ujenzi unaotarajiwa kukamilika
ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kuwataka kuwatumia vijana
wanaotekeleza mradi huo katika miradi mingine.
"Hili kundi la vijana walioshiriki kufanya kazi hii msiwaache, namimi
nitawapa majengo mpaka mtakimbia nyinyi wenyewe ntakuwa nikiwapa kazi,
hawa vijana wamejitoa kwa nguvu zao na ndiyo wanatakeleza dhana ya hapa
kazi tuu" alisema Dkt. Magufuli.
No comments:
Post a Comment