Tuesday, 4 October 2016

kikosi cha usalama barabarani kimeingizia Serikali kiasi cha jumla ya tozo Tsh 464,790000/=

 Image result for simon sirro
Na HERIETH SEMGAZA
Jeshi la Police Kanda Maalum  Dar es salam limesema  matukio ya kiuhalifu jijini humo yameanza kupungua hii ni kutokana na  kutumia mbinu ya  ulinzi shirikishi linaloundwa na kiongozi wa serikali za mitaa kwa kusaidiana na police kadhaa,ili kupunguza uhalifu.
Hayo yamesemwa na Kamishina wa Police Kanda Maalumu ya Dares salaam Kamanda Simon Sirro mkutano na waandishi wa habari  kituo cha kati jijini  Dar es salaam  wakati alipotaja  idadi ya matukio yaliyojitokeza hivi karibuni jijini humo.
Kamanda Siro amesema jeshi hilo limesikitishwa na uharibifu uliojitokeza siku ya tarehe 2 /10/2016 katika uwanja wa taifa ,nakueleza kuwa watafanya uchunguzi ili kubaini watu wote walioshiriki katika uharibifu huo na kuwafikisha mahakamani mara tu wanapokamatwa.
Kamanda Siro  ameongeza  kuwa jeshi la police kanda maalumu ya Dar es salaam kupitia kikosi cha usalama barabarani kimekamata makosa mbalimbali  kuanzia tarehe 27/9/2016 hadi tarehe 2/10/2016 na kuingizia serikali kiasi cha jumla ya tozo Tsh 464,790000/=
Pamoja na hayo amewaomba wananchi kuwa wepesi kutoa taarifa za kiuhalifu bila woga pindi wanapoziona au kusikia  ili jeshi la polisi liendelee na kazi kubwa ya kudhibiti na  kutokomeza uhalifu jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment