Wednesday 31 May 2017

Mbowe amzuia Mbunge lucy kuchangia bungeni

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe amesema alipopata taarifa ya kifo cha Mbunge wa zamani wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alijaribu kumzuia mtoto wa marehemu, Lucy Owenya asichangie bungeni  lakini alishindwa.
Mbowe ameyasema hayo leo Jumatano wakati akilitangazia bunge kuhusu kifo cha Mwenyekiti huyo wa Chadema, mkoa wa Kilimanjaro.
Owenya ni mbunge wa viti maalum wa chama hicho na mtoto wa kada huyo mkongwe wa Chadema.
 
 "Ilipofika zamu yake kuchangia nilimruka hata akalalamika inakuwaje wakati alitakiwa atoe maoni yake. Tushirikiane na familia ya marehemu ambaye alihudumu kwenye bunge hili kukamilisha taratibu zilizobaki," amesema Chenge.

No comments:

Post a Comment